WADAU WAKUTANA DAR KUJIFUNZA FURSA ZA UBIA
Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP Centre), kwa kushirikiana na Jukwaa la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), kimewakutanisha wadau kwa sekta binafsi jijini Dar es Salaam katika mafunzo maalum ya kujenga uwezo kuhusu miradi ya ubia (PPP).
Mafunzo haya yamelenga kutoa uelewa wa kina kuhusu namna Tanzania inavyoweza kutumia kikamilifu mfumo wa PPP kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hususan katika muktadha wa mabadiliko mapya ya sheria na fursa zilizopo kwenye orodha ya miradi (pipeline).
Kupitia majadiliano ya kitaalamu na uzoefu wa wataalam kutoka sekta binafsi, washiriki wamepata uelewa mpana juu ya nafasi ya sekta binafsi katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku wakihamasishwa kuchangamkia fursa za uwekezaji katika sekta za kimkakati.
Tranding News
Newsletter
Subscribe to our newsletter to get the latest news

