logo

'MPISHI WA NIGERIA' HILDA BACI AVUNJA REKODI YA KUPIKA

Juhudi za mpishi wa Nigeria kuvunja rekodi ya kupika kwa muda mrefu bila kukoma zimetambuliwa rasmi na Guinness World Records (GWR).

-

Hilda Baci alianza kuvuma nchini humo baada ya kupika kwa siku nne mwezi uliopita.

-

Alipika kwa saa 100 na aliruhusiwa mapumziko ya dakika tano kila saa.

-

Hata hivyo GWR imeweka rekodi yake kwa saa 93 na dakika 11, na kupunguza muda wa saa saba kwa alizochukua mapumziko.

-

Hilda anaipiku rekodi ya hapo awali kwa zaidi ya saa tano iliyowekwa huko Rewa, India 2019 na mpishi wa India Lata Tondon aliyepika kwa saa 87 dakika 45.

#JordanMediaupdates

Frank Jordan
12345 123
Follow Us
logo

© 2023 Jordan Media. All Rights Reserved. Designed by Lylical Popcorn