WATU 16 WAUAWA,400 WAJERUHIWA KWENYE MAANDAMANO YANAYOENDELEA NCHINI KENYA
Watu 16 wameuawa na takribani 400 kujeruhiwa baada ya maelfu ya watu kumiminika mitaani nchini Kenya siku ya Jumatano kuandamana dhidi ya serikali.
.
Shirika la Amnesty International Kenya limesema, Waandamanaji waliingia mitaani wiki hii kuadhimisha mwaka mmoja tangu maandamano ya kupinga ushuru Juni mwaka jana, ambayo yalisababisha vifo vya watu kadhaa na kuzua ghadhabu nchini kote.
Maandamano ya mwaka wa 2024 yalilazimisha kuondolewa kwa mswada wa fedha ulioibua kodi.
.
Hata hivyo, vijana wengi wa Kenya bado wamekasirishwa na visa kadhaa vya madai ya ukatili wa polisi, ikiwa ni pamoja na kifo cha mwalimu chini ya ulinzi wa polisi na kupigwa risasi kwa mchuuzi wa mitaani ambaye hakuwa na silaha.
Siku ya Jumatano, maelfu ya watu waliandamana katika mji mkuu wa Nairobi, mji wa pwani wa Mombasa na miji mingine kuadhimisha kumbukumbu ya maandamano hayo.
Jijini Nairobi, barabara zinazoelekea katika jengo la Bunge la Kenya na ofisi ya rais zilizuiliwa kabla ya maandamano hayo.
CNN ilishuhudia polisi wakifyatua risasi moja kwa moja jijini Nairobi kutawanya waandamanaji wa amani Jumatano huku mdhibiti wa serikali, Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya iliamuru vituo vyote vya televisheni na redio nchini kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya maandamano hayo yaliyoongozwa na vijana.
Tranding News
Newsletter
Subscribe to our newsletter to get the latest news

