MCHEZAJI VINICIUS JR ATABAKIA REAL MADRID HADI MWAKA 2032
Real Madrid imethibitisha rasmi kuongeza mkataba wa nyota wake Vinicius Jr., ambao sasa utamuweka klabuni hapo hadi Juni 30, 2032.
.
Vinicius alijiunga na Real Madrid mwaka 2018 akiwa na umri wa miaka 18 na tangu wakati huo amejiimarisha kuwa mmoja wa wachezaji muhimu zaidi katika historia ya mafanikio ya klabu hiyo.
.
Katika misimu minane aliyocheza, amecheza mechi 375, kufunga mabao 128 na kutwaa mataji 14.
.
Miongoni mwa mataji hayo ni Ligi ya Mabingwa Ulaya mara mbili, La Liga mara tatu, Kombe la Mfalme mara moja, Kombe la Dunia la Klabu mara tatu, Super Cup ya Ulaya mara mbili na Super Cup ya Hispania mara tatu.
.
Vinicius pia amekuwa na mchango mkubwa katika mafanikio hayo kwa mabao na pasi zake za mabao, ikiwemo kufunga katika fainali mbili za Ligi ya Mabingwa ambazo Real Madrid ilitwaa mwaka 2022 na 2024.
.
Mbali na mafanikio ya klabu, Vinicius ameshinda tuzo ya The Best ya FIFA mwaka 2024 na kutwaa tuzo nyingine kadhaa za kimataifa, huku akichaguliwa mara kadhaa katika kikosi bora cha dunia na cha Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Tranding News
Newsletter
Subscribe to our newsletter to get the latest news

