ACT-WAZALENDO YAPINGA MPINA KUONDOLEWA KUGOMBEA URAIS
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania imetengua uteuzi wa mwanasiasa Luhaga Mpina kuwa mgombea wa kiti cha urais kupitia chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo.
.
Vyombo kadhaa vya habari nchini humo vimeripoti kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya kuzuka mvutano wa ndani ya chama kuhusu taratibu zilizofanikisha Mpina kuwa mgombea siku chache baada ya kuhamia ACT Wazalendo akitokea chama tawala CCM.
.
Chama cha ACT kimesema kinaupinga uamuzi huo wa Msajili wa Vyama na kitafungua shauri mahakamani.
Frank Jordan
12345
123
Tranding News
Newsletter
Subscribe to our newsletter to get the latest news

